Je umekuwa ukijiuliza juu ya hukumu? Fuatilita somo
hili.
Fungu: (Ufunuo
20:12). "Nikawaona wafu wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti
cha enzi na vitabu vikafunguliwa na kitabu kingine kikafunguliwa ambacho ni cha
enzi na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile
vitabu sawa sawa na matendo yao."
Kumekuwa na dhana mbali mbali juu ya
hukumu. Wengine wamedai kuwa hakuna hukumu, wengine wakidai Mungu ana upendo
sana (jambo amblo ni kweli) na hivyo hawezi kuhukumu binadamu kifo hata ikiwa
wametenda dhambi. Wengine wamekuwa wakidhihaki huku wakidai hakuna kitu kama
hukumu kwani imemchukua Kristo miaka mingi na hadi leo hajarudi. Usichukuliwe
na dhana hizi mpendwa biblia ipo wazi na hata sasa hukumu inae
ndelea. (1 Petro 4:17) “Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje?”
Hukumu ni kwa waliotenda mema au
mabaya? ndelea. (1 Petro 4:17) “Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu; na ikianza kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje?”
(2 wakorintho 5:10) “Kwa maana imetupasa sisi sote
kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mtu apokee ijara ya
mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyotenda, kwamba ni mema au mabaya.”
Hivyo hukumu ni kwa wote watenda mema na mabaya. Danieli naye anaongezea katika
(Danieli 12:2) “ Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi
wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele.”
Hivyo wemgime watahukumiwa uzima wa milele huku wengine wakihukumiwa kifo yaani
aibu ya milele.
Danieli na vitabu vikifunuliwa kwa ajili ya hukumu
hiyo, (Danieli 7:9-10). “Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na
mmoja aliye mzee wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na
nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya
moto, na gurudumu zake moto uwakao. Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele
zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele
zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.
Ni watu wa umri gani watahukumiwa?
(Ufunuo 20:12) “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo,
wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu
kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika
mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.” Watu wa
rika zote watahukumiwa.
Je hukumu itahusisha mambo gani?
(Mathayo 12: 36) “Basi,
nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya
neno hilo siku ya hukumu”.
Siri zetu zote zitaletwa hukumuni, (Warumi 2:16) “katika siku
ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa
Kristo Yesu.”
(Muhubiri 12:13) “Hii
ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri
zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu. Kwa maana Mungu ataleta hukumuni
kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.”
Je inakuhitaji kuwa na dhambi kiasi
gani ili uhukumiwe kifo cha milele au uzima wa milele?
Dhambi moja tu hata iwe ndogo kiasi gani inaweza
kukusababishia usiingie kwenye ufalme wa Mungu. (Yakobo 2:20,11) “Maana mtu
awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa
juu ya yote. Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi
ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria.” (Mathayo 12:36). Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana,
watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.
Je tunawezaje kuepuka hukumu ya
kuangamizwa na kupotea juu ya uso wa nchi milele?
Walinaomtumainia Kristo, kumwamini na kushika maagizo yake na amri zake
ndio watakaokolewa. (Danieli 12:1) “Wakati huo Mikaeli atasimama, jemadari
mkuu, asimamaye upande wa wana wa watu wako; na kutakuwa na wakati wa taabu,
mfano wake haukuwapo tangu lilipoanza kuwapo taifa hata wakati uo huo; na
wakati huo watu wako wataokolewa; kila mmoja atakayeonekana ameandikwa katika
kitabu kile.”
Ingalipo
nafasi hatuna haja ya kuendelea lidumu katika dhambi. Hata kama tumefanya
dha,bi kiasi gani, ingalipo nafasi ya kutubu, Kristo anasubiri leo ufanye
maamuzi ya kuiacha dhambi ukajiunge na kundi la watakatifu watakaoishi milele
na milele baada ya zama zile za hukumu. Mpatanishi tunaye ambaye ni Yesu
Kristo. (1Timotheo 2:5) “ Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya
Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu.” (1 Yohana 1:9) “ Tukiziungama
dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na
kutusafisha na udhalimu wote.” Mungu aliahidi jambo kwa Isaya kuhusu wadhambi; (Isaya
1:18) “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa
nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera,
zitakuwa kama sufu.” (Isaya 45:25) “Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye
makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako.”
Ni
lini Kristo atakuja kuhukumu ulimwengu?
Siku Kristo
anapokuja haijuliani na ndio maana inatubidi muda wowote tuwe tayari,
hakunaanayejua maisha yake yatakoma lini (maana baada ya kufa hakuna njia
nyingne yoyote ya mwanadamu kuokolewa), wala hakuna ajuaye Kristo anakuja lini.
Hivyo basi yatupasa kujiweka tayari kila muda na kila wakati. (Mathayo 24:36) “Walakini
habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala
Mwana, ila Baba peke yake.”
Hivyo jiweke
tayari kumlaki Kristo ajapo mawinguni. Kwa nini usichague leo kumpokea Kristo
na kuishi kama apendavyo ili uepuke hukumu ya kifo cha aibu milele. Njoo leo
naye Kristo atakupokea
MUNGU AKUBARIKI UNAVYOTAFAKARI NENO LAKE
No comments :
Post a Comment